Witness (Wakilisha) na Ochuwanatarajia kupata mtoto
Msanii wa muziki wa Hip Hop, Witness ambae yupo kwenye mahusiano na msanii mwenzake Ochu Cheggy amesema kuwa ni mjamzito na anatarajia ...
https://mirindimoyapwani.blogspot.com/2014/05/witness-wakilisha-na-ochu-wanatarajia.html
Msanii wa muziki wa Hip Hop, Witness ambae yupo kwenye mahusiano na msanii mwenzake Ochu Cheggy amesema kuwa ni mjamzito na anatarajia kupata mtoto wa pili. Akizungumza na Enewz ya EATV leo kuhusu muziki wake na mahusiano yake, Witness, amesema yupo kwenye mahusiano na Ochu na anatarajia kupata mtoto hivi karibuni.
“Were doing music together as Ochuness, so huyo ni mchanganyiko wa Witness na Ochu. Tupo pamoja kwa muda mrefu na mahusiano yetu yatazaa mtoto,nina mimba,” alisema Witness Witness amesema kuwa, hawana haraka na mpango wa kuhalalisha mahusiano yao katika
kuingia katika ndoa, na wanafanya kila kitu taratibu kwa kuzingatia usemi wa mambo mazuri hayataki haraka. Pia Witness amewataka wadau wa muziki kukaa mkao wa kula kwani anatarajia kuachia wimbo ambao utaelezea mahusiano yao na mambo mengine.

