DISQUS SHORTNAME

TUZO ZA KILI 2013 /14: RIPOTIKAMILI

Mwisho wa ubishi ! Hatimaye kile kinyang ’ anyiro cha Tuzo za Muziki za Kilimanjaro 2013 /14 kimefikia tamati wikiendi iliyopita kwenye U...


Mwisho wa ubishi ! Hatimaye kile kinyang ’ anyiro cha Tuzo za Muziki za Kilimanjaro 2013 /14 kimefikia tamati wikiendi iliyopita kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar , Ijumaa Wikienda lina ripoti kamili ya
matokeo na kilichojiri nyuma ya pazia. .
NANI KASHINDA TUZO GANI ?
Tuzo ya kwanza ilikuwa ni kipengele cha Wimbo Wenye Vionjo vya Asili vya Kitanzania ambapo tuzo ilikwenda kwa Bora mchawi wa Dar Bongo Massive .
NI YOUNG KILLER
Tuzo ya pili ilikuwa ni ya Msanii Bora Chipukizi ambapo aliyeibuka mshindi ni dogo anayetokea Mwanza , Erick Msodoki

CHEZEA JAYDEE?
Tuzo ya tatu ilikuwa kwenye Kipengele cha Wimbo Bora wa Zouk /Rhumba , ngoma iliyoshinda ni Yahaya ya Judith Wambura
TAYARI DIAMOND KAKALISHA
Tuzo ya nne ilikuwa ni Kipengele cha Wimbo Bora wa Afro - Pop , tuzo ilikwenda kwa Ngoma ya Number One ya Nasibu Abdul ‘ Diamond Platnumz ’ akiwaangusha Lady Jaydee , Abdu Kiba na Ali Kiba , Kassim
Mganga na Rich Mavoko . Shabiki wa Diamond akimpongeza kwa kutwaa tuzo nyingi . Katika tuzo ya tano ilikuwa ni Kipengele Wimbo Bora wa Ragga ambapo Ngoma ya Nishai wa Chibwa akimshirikisha Juru.
Tuzo ya sita ilikuwa ni Kipengele cha Wimbo Bora wa Reggae ambapo Wimbo wa Na Wewe, mshindi alikuwa ni Dabo. Weusi wakiwa na tuzo yao ya Kikundi Bora cha Mwaka, Kizazi Kipya .
MZEE YUSUF KATISHA
Katika tuzo ya saba, ilikuwa ni Kipengele cha Wimbo Bora wa Taarab , ngoma iliyoibuka kidedea ni Wasiwasi Wako wa Mzee Yusuf . Msanii Bora wa Hip hop na Mtunzi Bora wa Mwaka Hip hop , Farid Kibanda ' Fid Q' baada ya kutwaa tuzo zake mbili.
JAHAZI KINARA
Tuzo ya nane ilikuwa ni Kipengele cha Kikundi cha Mwaka cha Taarab ambapo Jahaz Modern Taarab waliibuka kidedea. Msanii Young Killer akipokea tuzo yake ya Msanii Bora Chipukizi Anayeibukia kutoka
kwa msanii JB.
ISHA MASHAUZI NAYE
Katika tuzo ya tisa ilikuwa ni Kipengele cha Mwimbaji Bora wa Kike Taarab , mshindi alikuwa ni Isha Ramadhan ‘ Mashauzi
MZEE YUSUF TENA
Kwenye Kipengele cha kumi ilikuwa ni Mwimbaji Bora wa Kiume Taarab ambapo kama kawa Mzee Yusuf aliibuka kinara ikiwa ni tuzo yake ya tatu .
KWELI USHAMBA MZIGO
Kipengele cha kumi ilikuwa ni Wimbo Bora wa Kiswahili Bendi , wimbo bora ulikuwa Ushamba Mzigo wa Mashujaa Musica. Mtunzi Bora wa Mwaka Bendi , Christian Bella akipokea tuzo yake kutoka kwa Issa Michuzi .
HONGERA DA ’ LUIZA
Tuzo ya kumi na mbili katika Kipengele cha Mwimbaji Bora wa Kike Bendi, tuzo ilikwenda kwa Luiza Mbutu wa The African Band ‘twanga pepeta'
ASANTE JOSEE MARA
Katika kipengele cha kumi na tatu kilikuwa ni Mwimbaji Bora wa Kiume Bendi , tuzo ilikwenda kwa Josee Mara Bendi ya Mapacha Watatu akiwaangusha Chaz Baba , Kalala Junior, Khalid Chokoraa na Christian Bella.
FERGUSON HUREEE!
Tuzo ya kumi na nne ilikuwa katika Kipengele cha Rapa Bora wa Mwaka Bendi, tuzo ilikwenda kwa Saulo John ‘ Ferguso ’ wa Mashujaa Musica akiwaangusha Chokoraa , Kitokololo, Kanal Top na Totoo Zebingwa.
NI MASHUJAA MUSICA
Katika tuzo ya kumi na tano, kwenye Kipengele cha Bendi ya Mwaka, tuzo ilikwenda kwa Bendi ya Mashujaa Musica ikiwagaragaza Akudo Impact, Twanga Pepeta , FM Academia , Malaika Band na Mapacha Watatu.
LADY JAYDEE TENA
Tuzo ya kumi na sita ilikuwa ni Kipengele cha Mwimbaji Bora wa Kike Kizazi Kipya ambapo
Lady Jaydee aliwagaragaza Vanessa Mdee, Linah na Maua . Katika tuzo ya kumi na sana, ilikuwa ni Mwimbaji Bora wa Kiume Kizazi Kipya , mshindi alikuwa Diamond Platnumz akiwaangusha Ben Pol , Rich Mavoko , Ommy Dimpoz na Kassim Mganga huku akikabidhiwa tuzo hiyo na mpenziwe Wema
Isaac Sepetu na kuibua makelele ‘ oyooo .. .’ .
ARUSHA ‘ IN DA HOUSE ’
Katika tuzo ya kumi nane, Kipengele cha Kikubi Bora cha Mwaka cha Kizazi Kipya , ushindi ulikwenda kwa Weusi kutoka Arusha ambao walikabidhiwa tuzo hiyo na aliyekuwa shemeji yao kwa memba mwenzao , Lord Eyez, Rehema Chalamila ‘ Ray C ’ .
VANESSA CHUPUCHUPU
Wimo Bora wa RnB , ushindi ulikwenda kwa Closer wa Vanessa Mdee huku viatu virefu chupuchupu vikitaka kumuumbua. Kwa upande wa Wimbo Bora wa Hip Hop , tuzo ilikwenda kwa Ngoma ya Nje ya Box wa Nikki wa Pili wa Weusi .
FID Q JUUU !
Katika Kipengele cha Msanii Bora wa Hip Hop, tuzo ilikwenda kwa Fid Q ambaye alizingirwa kila upande . Kwenye Wimbo Bora wa Kushirikiana , tuzo ilikwenda kwa Wimbo wa Muziki Gani aliomshirikisha Diamond Platnumz.
WATUMBUIZAJI
Awali kulikuwa na shoo za madasa mbalimbali kisha akafuatia Faraji Nyembo ‘ Ommy Dimpoz’ na Bendi ya Motomoto.
EXTRA BONGO, TWANGA PEPETA
Baada ya hapo zilifuata burudani kutoka kwa Extra Bongo ‘ Wazee wa Kizigo ’ na Twanga Pepeta ambao kwa pamoja walionesha ‘ lavu ’ kwa kusalimiana.
WEUSI, MADEE
Baada ya dansi walipanda Weusi wakiongoza na Joh Makini ambao walivunja na ngoma yao kali ya Gere iliyowapandisha watu mizuka kisha kumpisha Hamad Ally ‘ Madee ’ akaburudisha kupitia ngoma yake ya Pombe Yangu. Baadaye alipanda jamaa ‘ mchaga ’ Fredy Saganda ‘ Mo ’ na ngoma yake ya zamani ya
Namna Gani kisha akaimba Wimbo wa Kiarabu na kusababisha ukumbi kurindima kwa shangwe na kutuza .
WASIOFIKA KUCHUKUA TUZO
Baadhi ya wasanii waliopata tuzo hawakufika kuchukua tuzo zao na badala yake walituma wawakilishi hivyo kula uso kuwa hawapendi kujumuika. Baadhi yao ni pamoja na Lady Jaydee na Mzee Yusuf . Kwa habari zaidi usikose Gazeti la Uwazi kesho Jumanne .

Related

HABARI YA MJINI 954835651569398224

Post a Comment

Comment zako Kuhusu hii stori

emo-but-icon

Hot in week

Recent

Comments

item