Master J KIKAANGONI LIVE: PRODYUZA WA DIAMOND ALISTAHILI TUZO,MAN WATER HAKUSTAHILI,AZUNGUMZIA NDOA YAKE NA SHAA
Producer mkongwe Joachim Kimaryo aka Master J ametoa mtazamo wake kuhusu tuzo za KTMA 2014 ambao unaonesha hakuridhishwa na mshindi wa tu...
https://mirindimoyapwani.blogspot.com/2014/05/master-j-kikaangoni-live-prodyuza-wa.html
Producer mkongwe Joachim Kimaryo aka Master J ametoa mtazamo wake kuhusu tuzo za KTMA 2014 ambao unaonesha hakuridhishwa na mshindi wa tuzo ya mtayarishaji bora wa mwaka – kizazi kipya ambaye ni Man Water wa Combinenga.
“Sijaelewa damond kupata tuzo 7 alafu produza wake kutoka na 0!!!!!” ni jibu la moja ya maswali kuhusiana na tuzo hizo aliyokutana nayo Master J Jana alipokuwa mgeni katika session ya ‘Kikaangoni Live’ kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV.
Shabiki mwingine aliuliza: “Pia man water ni mkali au unasemaje master J?”
Na hiki ndicho alichojibu Jay: “mkali lakini hakusahili kushinda mwaka huu”
Swali tofauti na muziki ambalo lilijirudia mara nyingi ni kuhusu uhusiano wake na mpenzi wake Shaa, shabiki mmoja aliuliza:
“Mnafunga ndoa lini ww na Shaa manake mnapendezana kweli? Au ni mchepuko tu wa lami?
Na jibu la Joachim aka Master J mabibi na mabwana lilikuwa “SOON”.


