DIDA AZUA TIMBWILI BAADA YAKUNG' ANG' ANIWA NAMWANAMKE MWENZAKE
DUNIA ina mambo! Prizenta wa Radio Times FM, Hadija Shaibu ‘ Dida’ amezua timbwili baada ya kung’ ang ’ aniwa na mwanamke mwenzake aliye...
https://mirindimoyapwani.blogspot.com/2014/05/dida-azua-timbwili-baada-ya-kung-ang.html
DUNIA ina mambo! Prizenta wa Radio Times
FM, Hadija Shaibu ‘ Dida’ amezua timbwili
baada ya kung’ ang ’ aniwa na mwanamke
mwenzake aliyedaiwa kutaka kumshawishi
afanye naye mapenzi ya jinsi moja ( usagaji) .
Prizenta wa Radio Times FM, Hadija Shaibu
‘ Dida’
Dida alikumbwa na ishu hiyo , Alhamisi ya
wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa Mango
Garden , Kinondoni jijini Dar , wakati Kundi la
Mashauzi Classic, lilikuwa likiangusha
burudani.
Katika tukio hilo lililoshuhudiwa na
‘ shushushu’ wetu, mwanamke huyo
aliyetajwa kwa jina moja la Addy ambaye
anadaiwa kukubuhu kwa tabia hiyo chafu ya
usagaji.
Ilisemekana kwamba mwanadada huyo
alianza kumzengea Dida kwa kumsemesha
huku akimuonesha pozi za kimahaba .
Licha ya mtangazaji huyo kumpuuza , Addy
alifika mbali na kuanza kumshtua kwa
kutokea nyuma yake kwa kumtekenya huku
akimkonyeza na kumshawishi waongee vizuri.
Kutokana na vitendo hivyo , Dida alipandwa
na hasira na kuchukua chupa kutaka
kumpasua ndipo Addy naye akawa
anahangaika kujitetea na kusababisha vurugu
katika eneo hilo, shukrani ziwaendee
wasamaria wema waliwatuliza .
Akizungumza na Risasi Jumamosi mara
baada ya kutulizwa , Dida alisema :
“Huyu dada ni muda mrefu alikuwa
akinisumbua hapa ukumbini, mwanzo
nilikuwa sijajua anachotaka kumbe ni
mshenzi kabisa , anataka kunifanya vitendo
vya kisagaji , amenikera sana. ”
