Mtoto wa Usher amemkosoa baba yake kwamba hajui kuimba
Usher Raymond ana heshima ya pekee kwenye muziki duniani, hasa kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuimba na kudance pia, lakini unamfahamu ‘do...
https://mirindimoyapwani.blogspot.com/2014/11/mtoto-wa-usher-amemkosoa-baba-yake.html
Usher Raymond ana heshima ya pekee kwenye muziki duniani, hasa kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuimba na kudance pia, lakini unamfahamu ‘dogo’ wa miaka 7 aliyemkosoa Usher kwamba hajui kuimba?
Mtoto wa Usher, Neyvid amewahi ‘kumchana’ baba yake kuwa anavutiwa zaidi na baba yake akiwa anacheza lakini sio akiwa anaimba.
“.. aliponiona nafanya show kwenye tour yangu iliyopita.. mara nyingi alikuwa anaangalia zaidi namna ninavyocheza.. Na kuna wakati namuona anaiga ninavyocheza..”—Usher.
Unakubaliana na mtoto wa Usher Raymond kwamba baba yake hajui kuimba?
