DISQUS SHORTNAME

SAGUDA AELEZEA MAISHA YAKE NA MAREHEMU MKEWE RACHEL

ILINICHUKUA muda kukikubali kifo cha rafiki  yangu kipenzi , mwigizaji Rachel Haule  ‘ Recho ’ ambacho kilitokea Mei 26 , mwaka huu katika...

ILINICHUKUA muda kukikubali kifo cha rafiki  yangu kipenzi , mwigizaji Rachel Haule  ‘ Recho ’ ambacho kilitokea Mei 26 , mwaka huu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili , Dar . Lakini sina cha kufanya. Ni kweli Recho ameondoka . Hapa nataka nizungumzie  kidogo maisha yangu na marehemu Recho
Kama inavyokuwa kwa wanadamu wengi kupitia changamoto maishani , Recho naye  alipitia mitihani ya hapa na pale ya kidunia lakini hakuvunjika moyo.
Alipambana  kuhakikisha ndoto zake za kuwa mwigizaji mkubwa Bongo na nje ya Bongo zinatimia . Kabla ya jina lake halijaanza kujulikana katika vyombo vya habari, Recho alikuwa  akijaribu kukaa karibu na mastaa wakubwa ili  aweze kupata uzoefu na baadaye kusimama mwenyewe kwenye sanaa.  Aliweka kambi ndani ya Kampuni ya RJ chini  ya wa uongozi wa Ray na Johari akajielimisha na kupata mwanga wa maisha  yake kisanii. Akaanza kuonekana katika
sinema chache za kushirikishwa . Aliuza kwenye sinema kubwakubwa kama  Danger Zone , Family Disaster, Long Hope ( haijatoka ) , Mke Mwema, Gentlemen , Cindy , Life to Life, Loreen , Uyoga, Men’ s Day Out ,Unpredictable na Figo ambayo alicheza na  Jennifer Kyaka ‘ Odama ’ .  Tangu hapo akaanza kushirikiana na mastaa wengine kama Jacqueline Wolper na wengine  kisha baadaye akakita nanga kwa rafiki yake
kipenzi, Odama wakaendelea kufyatua filamu mpya kila mwezi . Kwa kipindi chote hicho niweke wazi tu ,nilikuwa karibu na marehemu.Niweke wazi pia kuwa nilikuwa bega kwa  bega na mchumba wa marehemu, George Saguda. Tulikuwa tukishirikiana mambo  mengi kama vijana , naweza kusema  walikuwa hawanifichi kitu iwe ni cha kuhusu kazi au binafsi.  Kampani yetu ilikuwa ni ya shida na raha,marehemu na mchumba’ ke hawakuwa wakijisikia hata baada ya kuwa maarufu  katika jamii .  Ilikuwa ni suala la Recho au Saguda kunipigia simu na kuniambia tukutane , tunakutana kuzungumza, kushauriana huku pia tukinywa
na kufurahi. Ilikuwa ni rahisi Saguda au Recho kuniambia  kazi au mipango ya kufanya kazi sehemu
kabla ya kumwambia mtu yoyote. Hapa nakiri, kutokana na kazi yangu ya uandishi,  kuna wakati nilikutana na changamoto kubwa .  Recho na Saguda walikuwa nami bega kwa  bega na kunishauri mambo ya busara .
Naamini hata mimi yapo mengi mazuri ambayo katika kazi yao nimeweza  kuwashauri, wao wenyewe wanajua. Tulishaurina kama vijana . Kweli kadiri siku zilivyozidi kusonga mabadiliko kati yetu
yalianza kuonekana. Kama ujuavyo Waswahili , kutokana na ukaribu wangu na Recho , kuna wakati
yaliwahi kuibuka manenomaneno juu ya uhusiano wangu naye .  Tuliyapotezea kwani zaidi ya urafiki wa
kawaida , hakuna kingine cha ziada kilichoendelea kati yetu .  Nilimheshimu na nitamheshimu Recho .
Nilimheshimu na ninamheshimu sana Saguda. Naamini hata kama Saguda alisikia  uvumi uliomhusu mchumba’ ke na mimi ,  aliupotezea na kuuona wa kijinga kama nilivyofanya .Hata baada ya wawili hao kutofanya kazi kwa karibu na RJ ambapo mara nyingi tulikuwa tukikutana kuzungumza , tulikuwa
tukikutana kwenye viunga tofauti vya jiji,maisha yakiendelea. Mwezi mmoja uliopita nilikaa na Saguda
kwenye Ukumbi wa Eagle uliopo Sinza-  Mapambano , Dar .  Tulikunywa na kufurahi, hatukuzungumzia
kabisa ishu ya Recho ambaye muda huo nilikuwa nikijua ni mjamzito aliyebakiza siku  chache ajifungue ndiyo maana alikuwa haonekani kwenye viunga vyetu. Recho ambaye tulikuwa tukiwasiliana mara kwa mara kwa njia ya simu, alipopata taarifa ya kifo cha Adam Kuambiana hivi karibuni , alinipigia simu na kunieleza kwamba hataweza kwenda msibani kutokana na hali yake ya ujauzito .  Nilimwelewa lakini pia alinieleza jinsi marehemu Kuambiana alivyomtabiria jina la mwanaye mtarajiwa . Hapo ndipo nilipoandika habari katika gazeti hili wiki iliyopita kwenye ukurasa wa tatu iliyokuwa na kichwa cha habari; “Kuambiana
alimtabiria mtoto Recho .” Alimtabiria mtoto wa kiume , kweli ikawa hivyo lakini alifariki  dunia saa chache baada ya kujifungua kabla ya kufuata yeye. Wiki iliyopita , Recho alinisisitiza tuonane kwani mara nyingi alikuwa akipanga tuonane bila mafanikio . Alinieleza kuhusu ukimya na usiri wake wa kutangaza ujauzito katika vyombo vya habari kwani alihofia ndugu zake  kujua ikiwa bado alikuwa hajaolewa , aliogopa
aibu kama mtoto wa kike. Jumapili iliyopita nilimpigia simu kujua  anaendeleaje na lengo likiwa ni kutaka
kutimiza ahadi yetu ya kuonana , simu yake haikuwa hewani .  Hata nilipojaribu kupiga tena na tena , hakupatikana. Muda huo ndiyo alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Lugalo , Dar ,  akajifungua kisha kuhamishiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipoaga dunia.Inaniuma sana, lakini mbele yake nyuma yetu. Kwaheri rafiki kipenzi Recho . Pumzi kakwa amani !

Related

BONGO MOVIE 5817111388776765938

Post a Comment

Comment zako Kuhusu hii stori

emo-but-icon

Hot in week

Recent

Comments

item