DISQUS SHORTNAME

MKE WA KIGOGO AVUJISHA MESEJI ZA MAHABA ZA LULU

"Ni  muda mrefu nimekuwa nikifuatilia  mienendo ya mume wangu  kutokana na tabia yake kubadilika sana siku za hivi karibuni, nikabain...



"Ni  muda mrefu nimekuwa nikifuatilia  mienendo ya mume wangu  kutokana na tabia yake kubadilika sana siku za hivi karibuni, nikabaini kuwa kuna msichana anawasiliana naye kwa kutumiana meseji  za mapenzi, sikuwa na haraka nikaamua kufanya  uchunguzi wangu kimyakimya" "Wiki iliyopita mume wangu akiwa
amekwenda kuoga akasahau kuzima simu yake,na siyo  kawaida yake kuacha simu yake bila kuizima,mara
meseji ikaingia,nikaangalia nikaona jina la mtumaji amesevu Lulu, moyo ukalipuka" Ndivyo alivyoanza  kuongea mama mmoja  wa makamo  anayefanyakazi katika  ofisi moja  nyeti katikati ya
jiji la Dar alipokuja kuongea  na mwandishi wetu  wiki iliyopita baada ya ndoa  yake  kuingiliwa na mdudu
mbaya.... Akiongea kwa masikitiko makubwa, mama  huyo ambaye hakupenda kutaja jina lake  kutokana na unyeti wa  kazi anayoifanya, alidai  kuwa msichana huyo anayetaka kuiharibu ndoa yake yenye miaka 25 jina lake ni  Elizabeth Michael.... Mama huyo alidai kuwa jina hilo alilibaini baada ya kukuta meseji za
mapenzi kwenye simu ya mume wake na yeye kuamua  kuifuatilia namba hiyo kwa kufanya kama
anataka  kumtumia pesa msichana huyo na kukugundua jina hilo.... Akiongea kwa upole, mama huyo alidai kuwa katika  simu ya mume wake, jina la mtumaji  lilikuwa Lulu, lakini alipofanya uchunguzi wake wa
kujifanya kama anatuma pesa kwa namba ya msichana huyo ndipo alipobaini kuwa mmiliki  wa namba hiyo ni Elizabeth Michael... Mwandishi alimuuliza mama huyo kama anadhani kuwa msichana huyo
anayetaka kuiharibu ndoa yake ni muigizaji  maarufu wa filamu hapa nchini Elizabeth Michael "Lulu", lakini alikataa kuthibitisha hilo kwa madai kuwa  tangu siku hiyo namba ya binti huyo imekuwa haipatikani.... "Baada ya kugundua siku  ile , nilichukua simu  yake  na kutaka kuwasiliana naye ili niweze kumuonya  mwenyewe  kimyakimya kwa wakati wangu, wala sikuwa na lengo  la kuja kwenye  vyombi  vya habari , lakini sikuwahi kumpata hewani tena  kila nilipojaribu kumpigia"Alisema na kuongeza:
"Huenda mume  wangu alishtikia kuwa nimeona ujumbe ule, kwa sababu mimi nilipoisoma meseji ile sikuifuta, ili  akiona  meseji imesomwa aelewe nimeshajua kila kitu, pengine ndiye  aliyemwambia  binti huyo abadili namba yake" Mwandishi alimuomba mama huyo ampatie namba ya huyo msichana ili
kuweza kujua kama ni Lulu muigizaji ama siyo ( mwandishi anazijua namba zote za Lulu ), lakini namba hiyo ni tofauti na anazotumia Lulu Mwenyewe.... Mwandishi alipojaribu kama kumtumia pesa msichana huyo, jina
lililotokeza ni Elizabeth Michael, na alipojaribu kuipiga namba  hiyo ilikuwa haipatikani  hewani.... Juhudi  za kumsaka Lulu ili kuona kama anaitambua  namba hiyo hazikuzaa matunda kutokana na namba zake mbili kutopatikana na nyingine ikiita bila kupokelewa....
Angalizo:
Baadhi ya wasichana wa mjini wamekuwa  wakitumia majina ya wasanii maarufu katika nyendo zao
ili kuwatapeli watu. Miongoni  mwa njia wanazotumia ni pamoja na kujisajili kwenye mitandao ya kijamii kwa majina ya watu
maarufu ili kuwatapeli  watu.

Related

ZA MOTO 824021630937555762

Post a Comment

  1. Kuna tapeli wa fb anatumia no yenye usajili wa elizabeth michael ili kutapel watu atakua ni yeye afu ni mwanaume over

    ReplyDelete
  2. duuuh watu wabayaaa

    ReplyDelete

Comment zako Kuhusu hii stori

emo-but-icon

Hot in week

Recent

Comments

item